.
4th February, 2019
Uimarishaji wa huduma kwa wagonjwa wanaofika kwenye vituo vya afya unazidi kuboreshwa kila uchao. Na mojawapo ya njia za kuboresha huduma za matibabu ni kutumia teknolojia. Taifa la Thailand linatumia roboti kutoa dawa kwa wagonjwa mahospitalini. Wadadisi wamaswala ya teknolojia wanasema kuwa hii ni njia mwafaka sana ya kupunguza makosa na kuhakikisha kuwa mteja anapata dawa alizoandikiwa na daktari.