.
8th December, 2018
Mbio za Tsavo mwaka huu katika mbuga ya wanyama ya Tsavo Magharibi zimefanyika leo. Mbio hizo ziliandaliwa na wakfu ya urithi wa tsavo kwa ushirikiano wa washikadau ikiwemo kampuni ya standard group na hoteli ya sarova. Mbio hizi zinakusudia kuhamasisha watu kuhusu umuhimu wa kuhifadhi mazingira na kuchangisha pesa kwa mradi wa kusaidia kaunti zinazopakana na mbuga hiyo. Mwanahabari wetu sirajurahman abdullahi yuko katika eneo hilo na ametuandalia taarifa ifuatayo.