.
3rd September, 2018
Wavuvi sita ambao ni raia wa Kenya watafikishwa mahakamani nchini Uganda tarehe sita mwezi huu kujibu mashtaka ya uvuvi usio halali kwenye maji yaliyoko upande wa taifa la Uganda. Sita hao walikamatwa tarehe 24 mwezi agosti na maafisa wa uganda na kufikishwa katika kisiwa cha buvuma. Wavuvi kutoka ufuo wa nyan'gwina kaunti ndogo ya nyatike wametaja hatua hiyo kama unyanyasaji mkubwa. Kulingana na baba ya mvuvi mmoja anayezuiliwa na ambaye ni mwanafunzi wa kidato cha nne, wavuvi hao walikuwa wameenda kuvua ndani ya ziwa victoria wakati maafisa kutoka uganda walipo wakamata.