.
21st June, 2018
Waziri wa utalii Najib Balala amesitisha ufadhili wa bodi ya Brand Kenya kwa timu ya taifa ya raga ya wachezaji saba Shujaa. Hatua hiyo imefuatia tukio la hivi maajuzi ambapo wachezaji wa Shujaa waliamua kuziba nembo ya 'Make it Kenya' kwenye jezi zao katika mkondo wa Paris Sevens wakidai shilingi milioni 4 waliozokuwa walipwe kufuatia mkataba huo. Balala amesema kuwa jambo hilo limeidhalilisha Kenya ndiposa akachukua uamuzi huo.