.
16th January, 2018
Hali ya huzuni huku mamia ya waombolezaji wakijitokeza katika shule ya upili ya Ngai Ndeithia kaunti ya Nyandarua wakati wa mazishi ya watu tisa waliofariki kufuatia ajali kwenye barabara ya Nyeri – Nyahururu. Tisa hao walikuwa wakirejea nyumbani baada ya kuhudhuria mazishi eneo la Mukurweini kaunti ya Nyeri. Mazishi hayo yalihudhuriwa na viongozi mbalimbali ambao waliwataka wadau katika sekta ya usafirishaji kufanya hima huku wakiwataka madereva kuwa waangalifu ili kuepuka ajali za barabarani