.
24th September, 2016
Tukiwa bado katika taarifa za unadra wa maji Nairobi wakaazi wa mtaa wa NHC yaani National Housing Corporation eneo la Lang’ata vile vile wameathirika pakubwa na upungufu wa maji jijini wengi wakilazimika kununua maji kwani wanayapata maji kwa siku moja tu kwa wiki. Kutokana na gharama ya juu ya maji wakaazi hawa wameamua kuepuka gharama kubwa ya maji kwa kununua gari la maji. Maji hayo yanaweza kutosheleza kwa bei nafuu . Agnes Penda anaangazia taarifa hiyo kwa kina.