.
3rd September, 2016
Bingwa wa olimpiki katika mbio za mita 1500 upande wa kinadada Faith Kipyegon alirejea nchini kwa makaribisho ya aina yake, hii ikiwa ni baada ya kushiriki kwenye mbio za msururu wa almasi kule Zurich Alhamisi usiku. Msafara wake ulifika mjini Nakuru saa nne asubuhi na kupenyeza katikati mwa jiji alikolakiwa na gavana wa Nakuru Kinuthia Mbugua. Msafara huo uliendelea hadi kwao nyumbani katika kijiji cha Ndabiti eneo bunge la Kuresoi kusini ambako mamia ya jamaa na marafiki walikuwa wamekusanyika kumlaki.