Jumba jingine laporomoka Kariobangi lakini hakuna aliyejeruhiwa kwenye mkasa
2nd August, 2016
Wapangaji sita kwenye jumba moja eneo la kariobangi south jijini nairobi wameponea chupuchupu baada ya jengo lao la makazi kuporomoka. Jengo hilo la orofa tano liliporomoka saa mbili asubuhi ya leo. Kwa mujibu wa wakazi, lilitiwa alama ya kubomolewa lakini mmiliki akafuta alama hiyo ya “x”. Hakuna aliyejeruhiwa wala kupoteza maisha. Tukio likifanyika siku moja baada ya ukuta kuwaangukia na kuwaua watu watatu eneo la westlands, Nairobi.