Kifo cha “Maulana”: Makala maalum kuhusu kifo cha Jehovah Wanyonyi
7th June, 2016
Ni miezi saba sasa tangu kuibuka habari kwamba jamaa aliyedai kuwa mungu, Jehovah Wanyonyi amefariki. Licha ya hiyo habari kinzani hasa kutoka kwa wafwasi wake zimeibua mjadala na ugomvi kutoka magharibi ya nchi alikohudumu. KTN Leo imelizamia suala hilo hadi kufika kwenye kaburi lake na kuandaa makala maalum kifo cha maulana ambayo yanatoa ukweli wa iwapo alifariki ama la. Makala hayo yatapeperushwa katika sehemu ya pili ya taarifa hizi.