Wanafunzi zaidi ya 40 wanufaika kutokana na msaada wa masomo wa kaunti ya Nairobi
12th May, 2016
Wanafunzi 471 kutoka familia zisizojiweza kaunti ya Nairobi wamepokea mgao wa msaada wa elimu kutoka serikali ya kaunti. Msaada huo wa kima cha shilingi milioni 56 unatarajiwa kuwanufaisha wanafunzi kutoka shule za umma za baraza la jiji na zile za kaunti. Kila mwanafunzi akipokea mgao wa karo wa shilingi elfu hamsini na nne. Hafla hiyo iliongozwa na Waziri wa Elimu Kaunti ya Nairobi, Anne Lokidor.