Wahudumu wa matatu wapewa muda wa dakika 5 kuegesha magari katika vituo kati kati mwa jiji
12th April, 2016
Wahudumu wa matatu wamegadhabishwa na agizo la serikali ya kaunti ya Nairobi kwamba wana muda wa dakika 5 pekee kuegesha magari yao katika vituo vya kati mwa jiji ili kuwachukua abiria. Wahudumu hao wamesema hawatatii maagizo hayo kwani biashara zao zitaathirika pakubwa. Wakati huo huo serikali ya kaunti ya Nairobi imesema mpango huo ni wa kumaliza misongamano jijini.