Mto unaotegemewa na wakaazi wa Kibwezi waharibiwa na mafuta aina ya petroli
3rd November, 2015
Wakaazi wa kijiji cha Thange sehemu ya Kibwezi kaunti ya Makueni wamejawa na wasiwasi baada ya mto wanaoutegemea sana kwa maji ya kunywa kuharibiwa na mafuta aina ya petroli. Shule mbili zinasemekana kuathirika pakubwa na kufikia jioni hi, wakaazi wanadai tatizo bado lipo. Lakini katika mahojiano ya kipekee na mwanahabari wetu Francis Mtalaki kaimu mkurugenzi wa kampuni ya Kenya Pipeline asema tatizo hilo lilitatuliwa kwa siku moja.