Tembea Kenya: Kujivinjari kwenye mkahawa unaoelea baharini
9th October, 2015
Binadamu hutafuta njia mbalimbali za kujipa raha. Wengine wanapofika baharini kuogelea, wapo wanaojivinjari kwenye mikahawa inayoelea baharini na pia kupata uhondo wa kusafiri majini kwa jahazi huku wakipakuliwa vyakula na vinywaji. John Juma anatujuza zaidi kuhusu mkahawa uitwao the Moorings eneo la Mtwapa kaunti ya Kilifi kwenye makala yetu ya kila Ijumaa Tembea Kenya.