Uchaguzi wa maafisa wa ODM katika Kaunti wakumbwa na vurugu kwenye baadhi ya maeneo
6th October, 2015
Uchaguzi wa maafisa wa ODM katika Kaunti umekumbwa na vurugu kwenye baadhi ya maeneo. Leo katika Kaunti ya Kisumu utata uliibuka huku vurugu zikishuhudiwa katika ukumbi wa Tom Mboya Labor College. Kwa wakati mmoja mbunge wa zamani wa Muhoroni aliyekuwa akiwania uwenyekiti Ayiecho Olweny alifurushwa huku gari lake likipigwa kwa mawe. Mwanahabari wetu wa eneo la Nyanza Victor Ogalle anatuarifu zaidi.