Eneo la Kibiashara la Westgate lafunguliwa upya
18th July, 2015
Eneo la kibiashara la westgate linafunguliwa rasmi hii leo ikiwa ni takriban miaka miwili tangu shambulizi la kigaidi kufanyika hapo ambapo zaidi ya watu 67 waliuawa. Mapema wiki hii, gavana wa Nairobi- Evans Kidero, aliwatembeza wanahabari kwenye eneo hilo la kibiashara huku akitangaza kwamba sherehe rasmi za ufunguzi zitafanywa leo. Kauli za serikali kwenye hafla ya leo ya ufunguzi ni kwamba hatua ya kufungua rasmi eneo hilo la kibiashara imefanywa maksudi kuwasilisha ujumbe kwamba hawawezi kusimamsisha shughuli za Wakenya za kila siku .