Wahudumu wa afya wasusia kazi kulalamikia kucheleweshwa kwa mishahara yao Chuka
12th June, 2015
Huduma kwa wagonjwa katika hospitali kuu ya Chuka kaunti ya Tharaka Nithi zimelemazwa baada ya wahudumu wa afya wakiwemo madaktari, wauguzi na maafisa wa kliniki kususia kazi leo kulalamikia kucheleweshwa kwa mishahara yao. Wagonjwa katika kaunti ya Tharaka Nithi sasa wamelazimika kutafuta matibabu katika kaunti jirani za Embu na Meru. Francis Mtalaki ametuandalia taarifa hiyo kwa kina.