Watu kumi wafariki katika ajali ya Webuye-Eldoret
10th May, 2015
Watu 10 wamefariki katika ajali ya barabarani katika eneo la Kipkaren kwenye barabara ya Webuye - Eldoret. Ajali hiyo ilitokea mwendo wa saa tano asubuhi. Ajali hiyo ilihusisha matatu ya Kabras SACCO ambapo iliingia ndani ya trela. Matatu hiyo iliyokuwa na abiria 11 ilikuwa inaelekea Kakamega kutoka Eldoret. 7 walifariki papo hapo wengine 3 wakifariki wakiwa njiani kuelekea hospitalini. Majeruhi wanapokea matibabu katika hospitali ya wilaya ya Webuye na Eldoret.