Naibu Rais Wiliam Ruto atisha kufunga Kambi ya Wakimbizi ya Daadab
11th April, 2015
Serikali imeagiza kuhamishwa kwa kambi ya wakimbizi ya daadab hadi nchini somalia kama njia moja ya kukabili ukosefu wa usalama nchini. Naibu wa rais william ruto amesema kuwa kenya imeipa umoja wa mataifa miezi mitatu kuhamisha kambi hiyo la sivyo kenya ichukue hatua hiyo. Hatua hiyo imechukuliwa wakati ambapo kenya inatafuta mbinu a kukabiliana na kundi la alshabab ambao wamehusika katika mashambulizi likiwemo shambulizi la wiki jana katika chuo kikuu cha Garissa.