Mamia ya watu wafurika Chiromo kuomboleza waliouwawa Garissa
4th April, 2015
Shughuli ya upasuaji inatazamiwa kufanyika jumanne wiki ijayo ili kutambua maiti ambazo haziwezi kutambulika hii ni baada ya mpasuaji mkuu wa serikali johansen odour kutembela hifadhi ya maiti na kusema kuwa miili mingi haiwezi kutambulika bila ya kufanyiwa upasuaji. Kwa sasa ni miili 20 pekee ambayo imetambulika lakini kama anavyoripoti francis mtalaki familia moja ambayo imefanikiwa kumtambua mpendwa wao imesalia na majonzi tele baada ya kumpoteza msichana wa pekee waliokuwa na matarajio naye kuwa angebadilisha maisha ya familia hiyo.