Punda watano wapatikana mjini Nairobi katika barabara ya Kenyatta
30th March, 2015
Wakaazi wa Kaunti ya Nairobi hii leo waliamkia tukio la kushangaza lililohusisha punda watano waliokuwa wamefungwa katika barabara ya kenyatta hapa jijini nairobi. Punda hao waliokuwa na ujumbe ulioandikwa kwa rangi walidhamiriwa kupitisha ujumbe kuhusu hali ya ufisadi ilivyo humu nchini. Hata hivyo polisi wanawasaka watu waliowaacha punda hao barabarani.