×
× KTN KTN News KTN Morning Express KTN Leo Leo Mashinani The Big Story Checkpoint News Center E-Paper Lifestyle & Entertainment Nairobian Entertainment Eve Woman Travelog TV Stations KTN Home KTN News KTN Farmers TV Radio Stations Radio Maisha Spice FM Vybez Radio Enterprise VAS E-Learning Digger Classified Jobs Games Crosswords Sudoku The Standard Group Corporate Contact Us Rate Card Vacancies DCX O.M Portal Corporate Email RMS
Login
×
Show Swahili

Makamishna walioteuliwa na rais Uhuru kutafuta suluhu ya mzozo Makueni wahojiwa na kamati ya seneti

24th February, 2015

Kamati ya seneti kuhusu serikali za ugatuzi mapema hii leo iliwahoji makamishna walioteuliwa na rais Uhuru Kenyatta ili kutafuta suluhu ya mzozo unaoikumba kaunti ya Makueni Rais Kenyatta alipendekeza makamishna sita ambao wataongozwa na mwenyekiti wake Mohammed Nyaoga. Wengine watakaohusika katika shughuli hiyo ni mwenyekiti wa tume ya huduma kwa polisi Johnston Kavuludi , Emily Gatuguta , Profesa Harrison Mathioya , Alice Wairimu na wakili Taib Ali Taib. Kuhojiwa kwao kuliendelea kwa takriban saa sita huku kila mmoja wao akipata muda wa kuhojiwa. Mwezi wa Novemba mwaka jana , zaidi ya watu 3000 kutoka kaunti ya Makueni walikita kambi katika jumba la Harambee na kumkabidhi rais Kenyatta malalamishi yao kuhusiana na uongozi wa kaunti hiyo. Kamati hiyo inatarajiwa kutoa pendekezo lake hapo kesho.
.
RELATED VIDEOS