COTU wasikitikia mauaji ya Mbunge George Muchai
7th February, 2015
Maafisa wa Kaunti ya Nairobi wamesema kuwa kamera za CCTV katika eneo la mkasa wa mwenda zake mbunge wa kabete George Muchai, dereva wake na walinzi wawili zipo kazini. Wamesema kuwa picha hizo zimo mikononi mwa polisi kwa uchunguzi zaidi. Mbunge George Muchai aliuawa leo alfajiri katika mzunguko wa barabara ya kenyatta hapa jijini Nairobi alipokuwa ameandamana na familia yake kutoka mtaa wa Westlands.