Mwanaume apashwa tohara ya lazima katika kaunti ya Bungoma
16th January, 2015
Wenyeji wa mji wa Chwele katika kaunti ya Bungoma wamejionea kioja cha bure, wakati jamaa mmoja mwenye wake wawili alipokamatwa na umati kisha kulazimishwa kukabiliana na kisu cha ngariba. Inasemekana kuwa ugomvi wa kinyumbani kati ya jamaa huyo na mkewe wa kwanza ndio chanzo cha mwanamke huyo kumripoti mumewe kwa wazee wa jamii ya wabukusu kuwa hajatairiwa, akiifanya njia mojawepo ya kumtia adabu.