Msichana wa Chuo Kikuu auawa na mchumbaye
6th December, 2014
Miaka ya nyuma wazazi walikuwa wakiwatafutia watoto wao wapenzi wa kuwaoa pindi wanapotimu umri. Enzi hiyo inaonekana kuzidi kutokomea na kusahaulika wakati kizazi cha dot com kikizama kwenye mitandao kulitafuta penzi. Mwishoni mwa wiki jana msichana mwenye umri wa miaka 22 alidaiwa kuuawa na mpenziwe raia wa uingereza waliyekutana kwenye facebook.