Mwanafunzi wa kidato cha nne katika shule ya Otieno Oyoo afariki katika hali ya kutatanisha
25th October, 2014
Kijana mmoja katika shule ya wavulana ya otieno oyoo alizimia na kufariki alipokuwa akisoma kwa mtihani wa kitaifa hapo jana. Mwendazake austine agumba alikuwa mwanafunzi wa kidato cha nne na kulingana na familia yake hakuwa na dalili zozote za ugonjwa. Lakini kama anavyoripoti nicholas wambua, wenzake waliodinda kutajwa walisema kwamba alipigwa kofi na mwenzake na kuzimia.