Vikosi vya umoja wa Afrika AMISOM vinajiandaa kwa mashambulizi kuuteka Mji wa Barawe
4th October, 2014
Ikiwa siku kuu ya Idd katika nchi jirani ya Somalia, vikosi vya somalia na vile vya umoja wa afrika nchini humo amisom vinajiandaa kwa mashambulizi kuuteka mji wa barawe. Mji wa barawe ni mojawapo ya ngome za wanamgambo wa alshabaab na hii itakuwa ni mara ya kwanza kwa vikosi vya serikali ya somalia kufika katika eneo hilo tangu taifa hilo kusambaratika baada ya vita vya 1991. Mwanahabari mohamed mahmoud amewasili nchini somalia na kukita kambi na wanajeshi hao wa amisom, na atakuwa akituletea habari kuhusu vikosi vya AMISOM kuuteka mji huo uliosalia kuwa ngome imara ya wanamgambo wa Alshabaab.