Jamii ya Mijikenda limemtembelea Gavana Salim Mvurya na kumwomba masamaha
3rd October, 2014
Baraza la wazee wa jamii ya mijikenda leo limemtembelea gavana wa kwale salim mvurya na kumwomba masamaha kufuatia kisa cha mapema juma hili ambapo mtu mmoja wa jamii hiyo alimpiga kwa bakora. Wazee hao wakiwa na mwenyekiti wa baraza hilo joseph karisa mwarandu vilevile walimwarifu gavana mvurya kwamba tayari wamekutana na lengo karisa mdzomba ambaye aliwaomba waomba msamaha huo kwa niaba yake. Kwa upande wake gavana mvurya aliridhia kauli yake ya hapo juzi kwamba tayari ameshamsamehe lengo na wala hatowasilisha tuhuma dhidi yake mahakamani. Aidha gavana mvurya amewaomba wazee hao kuandaa mkutano kati yake na lengo karisa.