PEACE INITIATIVE: Wazee wa Jamii ya Agikuyu wakutana kuhubiri amani
28th September, 2014
Baraza la wazee kutoka jamii ya agikuyu wameanzisha kampeini ya kuhubiri amani na utangamano katika kaunti zote 47 za humu nchini. Wakiongozwa na mwenyekiti wao wa kitaifa wachira kiago wazee hao walizuru kaunti ya kilifi na kufanya mazungumzo ya amani na wazee kutoka jamii ya mijikenda, na wabajuni huku baraza hilo la wazee likisema kuwa chuki za kisiasa humu nchini zimechangia kuwepo kwa ghasia kama zilivyoshuhudiwa katika sehemu mbalimbali za humu nchini. Wazee hao waliitaka jamii kuheshimiana pamoja na kuahidi kufanya kazi na wazee wa kila jamii kwa lengo la kuhubiri amani.