Watu tisa waripotiwa kufariki katika ghasia za Kaunti ya Mandera
26th August, 2014
Watu 9 wamethibitshwa kufariki katika kata ya gofa wargadit, kaskazini mwa kaunti ya mandera kufuatia mapigano yaliozuka leo kati ya mbari za garre na degodia. mashambulizi ya hi leo yalitekelezwa katika miji mengine miwili ambapo inashukiwa watu wengi zaidi wamepoteza maisha yao. kulingana na naibu wa chifu eneo hilo, wakaazi wamekosa la kufanya baada ya mafisa wa usalama na mashirika ya misaada kukosa kufika.