Wamiliki wa magari ya uchukuzi wa umma wayapeleka magari yao kukaguliwa dakika za mwisho
31st March, 2014
Usafiri wa umma hueanda ukaathirika pakubwa ifikapo kesho asubuhi kutokana na kuwa idadi kubwa ya magari ya uchukuzi wa umma hayajawekwa vidhiti mwendo vipya kama ilivyotakiwa na serikali kufikia . Misongamano mikubwa ya magari ya uchukuzi wa umma ilidhihirika katika vituo vya ukaguzi vya serikali , huku wamiliki wa matatu wakipata pigo baada ya ombi lao la kutaka kuongezewa muda wa ukaguzi wa magari yao kutupiliwa mbali na mahakama.