Kijana abuni mtambo wa kuzalisha nguvu za umeme
17th January, 2014
Kwa maeneo mengi ya mashinani , kupata umeme huwa ni ndoto ya wengi . Lakini kwa wenyeji wa kijiji cha Kahinduini katika kaunti ya Murang’a . Ndoto hiyo imetimia baada ya mvulana wa umri wa miaka 22 kubuni mitambo ya kuzalisha nguvu za umeme . Kijana huyo aliyekamilisha masomo ya shule ya upili mwaka jana pia anazo ndoto nyengine ikiwemo kuunda gari la kutumia nguvu za umeme .