Waziri wa leba Kazungu Kambi aunga mkono kupitishwa kwa mswada wa NSSF
7th December, 2013
Waziri wa leba Kazungu Kambi ameunga mkono hatua ya bunge ya kupitisha mswada wa kuongeza kiwango cha fedha wanachopaswa kukatwa wakenya kwa hazina ya malipo ya uzeeni NSSF. Akizungumza hapa jijini Nairobi kambi ameipongeza hatua hiyo na kusema kwamba itamuwezesha kila mkenya kuwa na fedha za kutosha kujikimu kimaisha pindi anapostaafu. Ameapa kukabiliana na ufisadi katika wizara hiyo kwa kila hali ili kuhakikisha kwamba wakenya wanapata huduma cha kiwango cha juu katika shughuli zao za kila siku.