Mswada Wa Sheria Kuhusu Ushuru
30th July, 2012
Mswada wa Sheria Kuhusu Ushuru wa asilimia kumi na sita juu ya ubora wa bidhaa fulani, yaani VAT unaotarajiwa kupelekwa Bungeni hapo kesho unapingwa vikali na baadhi ya Wabunge. Na kutokana na hili ,Waziri wa fedha Njeru Githae huenda akakumbana na wakati mgumu baada ya Wabunge watatu kuapa kuzuia kujadiliwa kwa mswada huo ambao wanasema iwapo utapitishwa na kuwa sheria, mwananchi wa kawaida atakandamizwa na mfumko wa bei ya vyakula na bidhaa muhimu. Frank Otieno anayo taarifa hiyo.