.
12th April, 2012
Hali ya taharuki ilitanda katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa Jomo Kenyatta, pale maafisa wa GSU waliojihami walipowazuia wafanyakazi wa viwanja vya ndege kurejea kazini, hatua hii imejiri licha ya mahakama kubatilisha uamuzi wa hapo awali wa kuwafuta kazi wafanyi hao. Mapema hapo jana muungano wa wafanyakazi – Cotu ulisema kuwa hatua iliyochukuliwa na mamlaka hayo ya viwanja vya ndege kwa wafanyikazi wake haikuwa halali.