.
25th January, 2021
Katibu wa wizara ya usalama wa ndani Karanja kibicho ameandikisha taarifa ya malalamishi kwa idara ya upelelezi (DCI) kufuatia madai dhidi yake yaliyotamkwa na aliyekuwa gavana wa nairobi mike mbuvi sonko.
Kibicho amesema kuwa atapeleka kesi kortini kumshtaki sonko kwa kumchafulia jina. Kibicho amewataka wanasiasa wa mrengo wa tanga tanga kukoma kumhusisha na siasa chafu wanazoendeleza huku akiahidi kuwa atarejelea kauli zao zote wakimtaja na kuwa atawachukulia hatua za kisheria.