.
26th October, 2020
Kenya imeandikisha historia hii leo baada ya kuzinduliwa rasmi kwa Ripoti ya Jopo la Upatanisho, la kuwaleta pamoja wakenya ili kuepuka uhasama na mizengwe kabla, wakati na baada ya uchaguzi nchini. Ripoti hiyo ilizunduliwa katika ukumbi wa Bomas ambapo Rais Uhuru Kenyatta na mwenzake wa "handsheki" Raila Odinga waliongoza kuwarai viongozi kuikumbatia ripoti hiyo.