7th May, 2021
Waziri wa afya Mutahi Kagwe ametoa wito kwa wakenya kuwa waangalifu zaidi haswa kipindi hiki ambako aina nyingine ya korona kutoka India imeripotiwa nchini. Hii inajiri kipindi ambapo kiwango cha maambukizi nchini kimefikia asilimia 6.3 baada ya watu 568 kuripotiwa kuwa na virusi hivyo baada ya sampuli 9,029 kufanyiwa vipimo. Watu 173 wamepona kutokana na ugonjwa huo huku 130 kati yao wakiwa kutoka uangalizi wa nyumbani wagonjwa wengine1,086 wamelazwa hospitalini kutokana na korona huku 131 wakiwa katika vyumba vya watu mahututi. Watu 15 pia wamefariki kutokana na virusi hivi