×
× KTN KTN News KTN Morning Express KTN Leo Leo Mashinani The Big Story Checkpoint News Center E-Paper Lifestyle & Entertainment Nairobian Entertainment Eve Woman Travelog TV Stations KTN Home KTN News KTN Farmers TV Radio Stations Radio Maisha Spice FM Vybez Radio Enterprise VAS E-Learning Digger Classified Jobs Games Crosswords Sudoku The Standard Group Corporate Contact Us Rate Card Vacancies DCX O.M Portal Corporate Email RMS
Login
×
Show Swahili

Hali ya Korona: Waziri Mutahi Kagwe azungumzia Korona ya India, awataka wakenya kuwa makini zaidi

7th May, 2021

Waziri wa afya Mutahi Kagwe ametoa wito kwa wakenya kuwa waangalifu zaidi haswa kipindi hiki ambako aina nyingine ya korona kutoka India imeripotiwa nchini. Hii inajiri kipindi ambapo  kiwango cha maambukizi nchini kimefikia asilimia 6.3 baada ya watu 568 kuripotiwa kuwa na virusi hivyo baada ya sampuli 9,029 kufanyiwa vipimo. Watu 173 wamepona kutokana na ugonjwa huo huku 130 kati yao wakiwa kutoka uangalizi wa nyumbani wagonjwa wengine1,086 wamelazwa hospitalini kutokana na korona huku 131 wakiwa katika vyumba vya watu mahututi. Watu 15 pia wamefariki kutokana na virusi hivi

.
RELATED VIDEOS