7th May, 2021
Uongozi wa Bunge la Taifa umetoa onyo kwa Naibu Rais William Ruto kwamba kutokana na kura ya jana ya kupitisha BBI bungeni, wana idadi tosha ya kuendesha mjadala wa kumwondoa madarakani. Viongozi hao wanasema hatua hiyo itachukuliwa iwapo hatakoma kudhalilisha uongozi wa Rais Uhuru Kenyatta.