5th June, 2020
Huenda wanafunzi wakaendelea kusalia nyumbani kwa muda mrefu zaidi, baada ya waziri wa elimu Profesa George Magoha kuonekana kuashiria shule hazitafunguliwa wakati idadi ya visa vya maambukizi ya virusi vya corona inaendelea kuongezeka. Waziri magoha alizungumza wakati alipokuwa akipokea ripoti ya kamati ya dharura ya kuratibu masuala ya elimu wakati huu wa janga la covid utakaowasilishwa rasmi kwa Rais Uhuru Kenyatta