×
The Standard Group Plc is a multi-media organization with investments in media platforms spanning newspaper print operations, television, radio broadcasting, digital and online services. The Standard Group is recognized as a leading multi-media house in Kenya with a key influence in matters of national and international interest.
  • Standard Group Plc HQ Office,
  • The Standard Group Center,Mombasa Road.
  • P.O Box 30080-00100,Nairobi, Kenya.
  • Telephone number: 0203222111, 0719012111
  • Email: [email protected]
Premium

KUPPET yazitetea shule zilizoimarika katika KCSE, 2022

News

Chama cha Kitaifa cha Walimu wa Shule za Upili na Vyuo vya Kadri KUPPET kimezitetea baadhi ya shule ambazo matokeo yake ya mitihani ya Kitaifa ya Kidato cha Nne mwaka jana, yaliimarika pakubwa kulinganishwa na awali.

Katibu Mkuu wa Chama hicho Akello Misori, amesema kuna uwezekano mkubwa kwa matokeo ya watahiniwa kutofautiana kila mwaka kutokana na sababu mbalimbali; mfano kuimarisha hali ya masomo na hata kubadilishwa kwa walimu na wakati mwingine watahiniwa kuwa werevu kulinganishwa na watangulizi wao.

Akihojiwa katika Spice FM Misori Misori amesema hatua ya watu kuibua maswali kuhusu matokeo mazuri kunaweza kuwafanya walimu na watahiniwa kufa moyo.

Kulingana naye hakuna tatizo lolote na matokeo ya shule zilizoimarika mwaka jana kwa kuwa hakuna visa vyovyote vya udanyanyifu vilivyoripotiwa.

Kauli hii inajiri wakati ambapo maswali mengi yamekuwa yakiulizw akuhusu matokeo ya shule za upili ya mwaka jana katika kaunti za Kisii na Nyamira.

Baadhi ya matokeo ambayo yameibua masuala ni ya shule ya Kitaifa ya Nyambaria iliyo katika Kuanti ya Nyamira iliyoibuka bora kitaifa ambapo watahiniwa mia nne kumi na mmoja wlaipata alama ya A katika mtihani wa 2022 kulinganishwa na 83 mwaka 2021. Shule nyingine ni ile ya Mobamba iliyoko Kaunti ya Kisii ambayo katika matokeo ya mwaka jana kulikuwa na watahiniwa wanne waliopata alama ya A kulinganishwa na mwaka 2021, na 2020 ambapo hakuna mtahiniwa hata mmoja aliyepata alama hiyo.

Related Topics


.

Trending Now

.

Popular this week