Washukiwa wa wizi KCB wakamatwa

Na, Beatrice  Maganga
Washukiwa wa wizi KCB wakamatwa
 
Polisi wamewatia mbaroni watu watatu kwa kuhusishwa na wizi wa shilingi milioni hamsini katika Benki ya KCB tawi la Thika. Mkuu wa Polisi Kaunti ya Kiambu, Adiel Nyange amethibitisha kukamatwa kwao huku akiahidi kufanyika kwa uchunguzi zaidi.
Katika taarifa iliyorekodiwa na Meneja wake katika Kituo cha Polisi cha Thika, Samuel Nganga, aliwasili katika benki hiyo asubuhi na kubaini fedha zilizowekwa katika chumba maalum zikiwa zimeibwa. 
Waliotekeleza wizi huo wanadaiwa kulichimba shimo chini ya ardhi hadi benki hiyo na kutekeleza wizi huo. 

Related Topics