Mahakamani
COFEK yawasilisha kesi kupinga uchujaji wa makatibu wa wizara
Shirika la Kutetea Maslahi ya Watumizi Bidhaa - COFEK limewasilisha kesi mahakamani kupinga jinsi shughuli ya kuwachuja makatibu wa wizara ilivyoendeshwa. Kupitia wakili wake Henry Kurauka, Shirika hilo limeambia mahakama kuwa tume ya huduma za umma PSC ilikiuka sheria katika uendeshaji wa shughuli hiyo. Katibu wa COFEK Stephene Mutoro ameiambia Radio Maisha kwamba PSC ilidinda kujibu barua ya COFEK kutaka PSC kujumuisha umma katika shughuli hiyo. Aidha COFEK imeiambia mahakama kuwa PSC haikuchapisha majina ya waliowasilisha maombi ya nyadhifa hizo. Kadhalika COFEK imedai kuwa PSC imewasilisha majina 66 ya waliopendekezwa kwa Rais. Jaji Isaack Lenaola ameagiza kusikizwa Jumatano tarehe 22 mwezi huu wa Mei.
Posted on May 21, 2013 na Carren Omae
