PODCASTS

Habari

  • Uchunguzi

    Jaji Barasa kuachishwa kazi

    Jopo lililoteuliwa kuchunguza mienendo ya Naibu jaji Mkuu Nancy Barasa limemshauri Rais Mwai Kibaki kumwachisha kazi jaji huyo. Mwenyekiti wa jopo hilo Jaji Mkuu mustaafu wa Tanzania Augustino Stephen Lawrence Ramadhan amesema uchunguzi wa jopo lake umebaini kwamba jaji Barasa alikiuka kanuni za afisi ya jaji kwa kumfinya pua na kumtishia maisha bawabu Rebecca Kerubo. Ikumbukwe kuwa rais Mwai Kibaki alimsimamisha kazi kwa muda Nancy Barasa tarehe 26 mwezi januari mwaka huu na kubuni jopo maalum la kuchunguza mienendo yake. Hatua ya rais Kibaki ilifwatia pendekezo la tume ya huduma za mahakama JSC. Jopo hilo la watu saba linajumuisha, Proffesa Judith Mbula Behemuka, jaju mtaafu Philip J. Ransley, Surinder Kapila, Beauttah Alukhava Siganga, Grace Barbara Ngele Madoka na Profesa Mugambi Jesse Ndwiga Kanyua.

    0 Responses

    Posted on August 6, 2012 na Mate Tongola

Comments in chronological order (Total 0 comments)



1100 characters remaining