Ufisadi
Ulaghai Isiolo
Kumechipuza madai ya ulaghai wa fedha Mjini Isiolo unaodaiwa kutekelezwa na maafisa wa Wizara ya Makao. Mkazi wa eneo hilo Mohammed Abdulahi anadai kuwa kuna afisa ambaye amekuwa akichukua fedha kutoka kwa wenyeji akiahidi kuwapa nyumba za serikali kwa bei ya chini. Tulifaulu kumpata afisa huyo kwa jina Nyamu Kiria na amejitetea vikali akisema hajashiriki ulaghai wowote.
Posted on August 2, 2012 na Mate Tongola
