PODCASTS

Habari

  • Moto

    Kiwanda Chashika Moto-Dandora

    Mali yenye thamani isiyojulikana imeteketea baada ya kiwanda cha kutengenezea magodoro kushika moto katika Mtaa wa Dandora hapa jijini. Inaarifiwa kuwa moto huo ulianzia katika chumba kimoja kabla ya kuenea katika vyumba vingine na kuteketeza magodoro kiwandani humo. Maafisa wa polisi wanasema huenda moto huo ulisababishwa na hitilafu za nguvu za umeme. Hakuna yeyote aliyejeruhiwa katika kisa hicho.

    0 Responses

    Posted on July 15, 2012 na Zaubeida Koome

Comments in chronological order (Total 0 comments)



1100 characters remaining