PODCASTS

Habari

  • Mahakamani

    Adai Mutula ni baba ya mwanawe

    Mahakama kuu imeagiza kuchukuliwa kwa chembechembe za DNA kutoka kwa mwili wa marehemu seneta wa Makueni Mutula Kilonzo kufuatia agizo la mwanamke kwa jina Eunice Nthenya anayedai kuwa marehemu ni baba mzazi wa mwanawe wa umri wa miaka 7. Jaji Luka Kimaru amesema kuwa chembechembe hizo zitatumika kubaini baba mzazi wa mtoto huyo kwenye kesi iliyowasilishwa mahakamani kupitia chama cha mawakili wa kike FIDA. Nthenya anasema kuwa ni yeye ni mwanawe mmoja wa wafanyikazi wa mwendazake na kwamba alijifungua kijana huyo tarehe 6 mwezi Mei mwaka 2006.

    0 Responses

    Posted on May 8, 2013 na Mate Tongola

  • ICC

    Kesi dhidi ya Ruto na Sang zahairishwa

    Tarehe ya kusikizwa kwa kesi dhidi ya naibu rais William Ruto na mtangazaji Joshua Arap Sang katika mahakama ya ICC itatangazwa jumanne wiki ijayo. Katika taarifa kwa vyombo vya habari, ICC imesema kuwa imeitisha kikao na pande husika ili kuamua siku tarehe mpya ya kusikizwa kesi hizo. Awali, kesi ya wawili hao ilikuwa imeratibiwa kuanza tarehe 28 mwezi huu. Kwenye kikao cha jumanne washirika watatarajiwa kutoa mchango wao kuhusu hatua ya kiongozi wa mashtaka wa ICC kutaka kuongeza mashahidi watano zaidi kwenye kesi hiyo. Mahakama hiyo vile vile itandaa kongamano la faragha na upande wa kiongozi wa mashtaka hii leona upande wa mawakili anaotetea watuhumiwa jumanne ijayo kujadili masuala yanayofungamana na kesi hizo.

    0 Responses

    Posted on May 7, 2013 na Victoria Amunga

  • Usalama

    19 kufikishwa kizimbani - Bungoma

    Washukiwa 19 waliokamatwa baada ya kuhusishwa na mashambulizi yaliyoshuhudiwa katika kaunti za Bungoma na Busia wanafikishwa mahakamani jumanne. 19 walikamatwa katika oparesheni ya polisi iliyoanza jumapili wiki iliyopita kufuatia mashambulizi ambayo yamesababisha vifo vya watu 8 na wengine zaidi ya 100 kujeruhiwa. Haya yanajiri wakati inspekta mkuu wa Polisi David Kiamiyo amedokeza kuwa polisi wanawanawachunguzi wanasiasa kadhaa ambao hawakutajwa kwa kuhusishwa na ghasia hizo. Aidha, Naibu rais William Ruto amevitaka vikosi vya polisi kuhakikisha kuwa waliohusika wanachunguzwa na kuchukuliwa hatua kali za kisheria.

    0 Responses

    Posted on May 7, 2013 na Mate Tongola

  • Mataifa

    Kusaidia Kujenga upya Somalia

    Rais Uhuru Kenyatta ni miongoni mwa viongozi kutoka barani Afrika na mataifa mengine wanaohudhuria kongamano la kujadili hatma ya taifa la Somalia linaloendelea jijini London. Kongamano hilo lililoanza mapema jumanne linaongozwa na waziri mkuu wa Uingereza David Cameron na rais wa Somalia Sheikh Hassan Mohamud. Katika hotuba yake, rais Mohamud amesema kwamba japo suluhu ya mzozo unaoshuhudiwa nchini Somalia ni raia wa taifa hilo wenyewe, usaidizi kutoka mataifa ya kigeni ni wenye umuhimu mkubwa. Aidha, kiongozi huyo ametowa wito kwa mataifa ya kigeni kulisaidia taifa lake lisitumbukie tena katika lindi la machafuko na ukosefu wa usalama. Wengine wanaohudhuria kongamano hilo ni rais wa Uganda Yoweri Museveni na wajumbe kutoka Afrika kusini, Umoja wa bara Afrika, Mauritius na Nigeria.

    0 Responses

    Posted on May 7, 2013 na Mate Tongola

  • Utawala

    Gavana Kidero alitangaza baraza lake

    Gavana wa kaunti ya Nairobi Evans Kidero ametaja baraza lake kuu la kaunti watakaofanikisha ndoto yake ya kuimarisha uchumi na ustawi wa kaunti ya Nairobi. Kwenye orodha hiyo ya idara 14; Silvanus Mwakaningo amechaguliwa kusimamia masuala ya fedha na Uchumi, Annae Kamis atasimamia idara ya Kilimo, John Wanyama Elimu, Ann Othoro kusimamia Biashara na Utalii, Daktari Timothy Kingondi kusimamia idara ya Afya, Gad Awuonda atashughulikia masuala ya Sheria huku idara ya mawasiliano na teknolojia ikiongozwa naye Mohammed Abdullahi. Aidha, aliyekuwa katibu wa baraza hilo John Gakuo amechaguliwa kongoza idara za Maji na mazingira na mali asili. Festo Fadamula ameridhika na wadhifa wa masuala ya kisiasa naye Ngure Mwaniki akitarajiwa kumshauri kimailifu gavana huyo kuhusu masuala ya uchumi.

    0 Responses

    Posted on May 7, 2013 na Caren Omae

  • Mishahara

    COFEK - Wananchi kukwepa ushuru?

    Shirika la kutetea haki za wateja COFEK limesema huenda likawashinikiza wananchi kukwepa ulipaji ushuru iwapo wabunge watafaulu katika azimio lao la kupata nyongeza kwa mishahara. Kwenye kikao na wanahabari, katibu wa COFEK Stephen Mutoro amesema kuwa wabunge wanastahili kufahamu kwamba si lazima mishahara yao iwe sawa na ya wabunge wa bunge la kumi. Shirika hilo pia limesema huenda likaanza kampeni za kuwashinikiza wakazi wa maeneo bunge ya wabunge walio mstari wa mbele kushinikiza nyongeza ya mishahara ili wasiwachague tena.

    0 Responses

    Posted on May 7, 2013 na Beatrice Maganga

  • Usalama

    Usalama wa jiji la Nairobi wajadiliwa

    Gavana wa Nairobi Evans Kidero anakutana na wakuu wa polisi kutoka eneo la Nairobi kujadili suala tata la usalama hususan kati kati mwa jiji. Miongoni mwa wanaohudhuria mkutano huo ni mkuu wa polisi eneo la Nairobi Benson Kibui na OCPD wa kituo cha Central Patrick Oduma. Wengine wanaohudhuria mkutano huo unaoendelea katika ukumbi wa baraza la jiji ni wadau kutoka sekta mbali mbali ikiwemo ya biashara ya na uchukuzi. Baadhi ya masuala ambayo tayari yamejadiliwa ni mbinu za kuponguza msongamano wa magari jijini.

    0 Responses

    Posted on May 7, 2013 na Mate Tongola

  • Mgomo

    Walimu watishia Kugoma

    Shule za umma zinafunguliwa kwa muhula wa pili jumatatu huku walimu wakitishia kugoma baada ya mazungumzo kati yao na Tume ya kuwaajiri walimu, TSC kuhusu nyongeza ya mishahara kusambaratika. Mwenyekiti wa KNUT Wilson Sossion amedokeza kuwa; kwenye mkataba wa mwaka 1997 kati yao na serikali, walimu walipaswa kutengewa kima cha shilingi bilioni 24 kila mwaka ingawa serikali ya NARC ilitupilia mbali na kukiuka mkataba huo mwaka 2003. Iwapo mkataba huo ungetekelezwa, mwalimu wa daraja la chini zaidi angepokea mshahara wa shilingi 16,692 kila mwezi na shilingi 11, 616 kama marupurupu.

    0 Responses

    Posted on May 6, 2013 na Mate Tongola

  • Bungeni

    Umma kuwasilisha malalamishi dhidi ya walioteuliwa

    Wananchi wamesalia na siku moja tu kupinga kwa kutoa sababu, orodha ya walioteuliwa na rais Uhuru Kenyatta kuhudumu katika baraza la mawaziri. Karani wa bunge la taifa Justin Bundi amedokeza kuwa bunge linaendelea kupokea maoni hayo kupitia barua au anwani (clerk@parliament.go.ke) Kwa mujibu wa kifungu cha 6 ibara ya 9 ya sheria kuhusu kuchaguliwa kwa afisa wa serikali, umma una uhuru wa kutoa maoni kuhusu walioteuliwa kabla ya wao kuchujwa na kamati ya bunge na kisha kuapishwa rasmi. Malalamishi hayo yatawasilishwa mbele ya kamati ya bunge kuhusu uteuzi ambayo imeratibiwa kuwahoji mawaziri hao 16 kati ya alhamishi na jumamosi wiki hii kabla ya kuwasilisha mapendekezo yao bungeni. Aidha, kuambatana na matakwa ya katiba, mahojiano ya 16 hao yanapaswa kuwa wazi kwa umma ingawa wanakamati hao 28 wanaweza kufanya mahojiano hayo faraghani iwapo mtahiniwa atapendekeza hivyo.

    0 Responses

    Posted on May 6, 2013 na Mate Tongola