ICC
UN haina usemi katika kesi za ICC, LSK
Huku habari zikichipuka za kuonyesha kwamba huenda serikali ya jubilee imeanza kutoa misimamo tofauti kuhusu suala la ICC, Mawakili wa humu nchini sasa wanasema kwamba Umoja wa Mataifa hauna uwezo wa kuingilia utaratibu wa kesi katika Mahakama hiyo. Mwenyekiti wa LSK Eric Mutua amesema kwamba almradi kesi zimeanzwa kusikizwa katika mahakama hiyo umoja wa mataifa una uwezo wa kuomba tu kuahirishwa kesi. Mwenyekiti huyo ameyasema hayo siku moja tu baada ya wakili wa naibu Rais William Ruto, Karim Khan, kunukuliwa akisema kwamba waraka uliowasilishwa katika umoja wa mataifa haukuwakilisha msimamo wa serikali. Khan amesema mteja wake anaheshimu majaji wa ICC na hawezi kuunga mkono hatua kama hiyo. Aidha LSK inasema hatua hiyo inaashiria kuwa waraka uliotumwa umoja wa mataifa unakosa uzito.
Posted on May 10, 2013 na Apopo Mujema
