PODCASTS

Habari

  • Wagonjwa

    Warejea Hospitalini - Mathari

    Wagonjwa watano zaidi waliotoroka kutoka hospitali ya wagonjwa wa akili ya Mathari hapa Nairobi wamerejeshwa hospitalini humo na jamaa zao. Kufikia sasa, idadi ya wagonjwa waliorejea ni 14 kati ya 40 waliotoroka hospitalini humo mapema wiki hii. Wasimamizi wa hospitali hiyo wametoa wito kwa umma wakiwemo wazazi wa wagonjwa 26 ambao kufikia sasa hawajulikani waliko, kuwarejesha hospitlaini ili waweze kuendelea kupokea matibabu.

    OCPD wa Starehe Samuel Anampiu ameiambia Radio Maisha kwamba 40 hao walikuwa miongoni mwa 75 waliotoroka kutoka chumba walimokuwa wamefungiwa. Hata hivyo, 35 kati yao walikamatwa baada ya jaribio lao la kutoroka kutofua dafu. Aidha, tisa kati ya waliotoroka walirejeshwa hospitalini humo na jamaa zao mapema jumatatu, huku 7 wakijirejesha wenyewe.

    0 Responses

    Posted on May 15, 2013 na Mate Tongola

  • Usalama

    Mkenya Atekwa Nyara Yemen

    Raia mmoja wa Kenya ametekwa nyara na waasi kusini mwa taifa la Yemen. Mkenya huyo anayefanya kazi na kamati ya mataifa ya shirika la Msalaba Mwekundu ni miongoni mwa watu watatu waliotekwa nyara na waasi hao waliokuwa na silaha. Taarifa zinasema watu wengine wanaozuiliwa na waasi hao ni raia wa Uswizi na mkalimani raia wa Yemen aliyekuwa akifanya kazi na wawili hao. Kufikia sasa, waasi hao hawajaelezea matakwa ya ukombozi wala sababu za kuwateka nyara watatu hao.

    0 Responses

    Posted on May 14, 2013 na Mate Tongola

  • ICC

    Ruto aelekea The Hague

    Mahakama ya ICC leo hii inatarajiwa kuandaa kikao cha kutathmini kesi dhidi ya Naibu Rais William Ruto na Mwanahabari Joshua Arap Sang. Ruto ambaye anataka mahakama hayo kuahirisha kesi dhidi yake hadi mwezi Novemba mwaka huu, anaarifiwa kuondoka nchini jumatatu usiku kuelekea The Hague Uholanzi kuhudhuria kikao hicho. Kwenye ombi lake kupitia wakili Karim Khan, naibu rais aliitaka mahakama kuahirisha kesi dhidi yake ili kutoa fursa kwa mawakili wake kujitayarisha ikizingatiwa kuwa upande wa mashtaka ulidinda kufichua mashahidi kwenye kesi hiyo. Haya yanajiri wakati mwanasheria mkuu wa Serikali Githu Muigai akidokeza kuwa atasafiri kuelekea Uholanzi kuhudhuria mkutano wa mataifa yaliyotia saini Mkataba wa Roma ili kujadili majukumu yao katika kufanikisha mkataba huo.

    0 Responses

    Posted on May 14, 2013 na Mate Tongola

  • Mishahara

    Wapinga Nyongeza ya Mishahara

    Mashirika ya jamii yameanda maandamano jumanne jijini Nairobi ambapo yamewalinganisha wabunge wa Kenya na nguruwe ikiwa hatua ya kupinga njama zao za kujiongezea mishahara. Aidha mashirika hayo yamekosoa vikali mpango wao wa kutaka kuibandua tume ya mishahara, SRC. Maandamano hayo yaliyowashirikisha wanaharakati kutoka mashirika mbali yakiwamo Transparency International, MUHURI na mengineyo, yalianzia katika bustani ya Uhuru na kutia nanga nje ya majengo ya bunge. Kulizuka kizaza wakati waandamanaji hao walipowafungulia nguruwe zaidi ya 10 kwenye lango la bunge, kuashiria ulafi wa wabunge wa Kenya. Hata hivyo, polisi walitumia vitoza machozi, na malori ya kuvurumisha maji, na mbwa kuwafurusha mamia ya waandamanji hao. Maandamano haya yanajiri siku chache baada ya rais Uhuru Kenyatta kuzungumzia suala la mishahara ya wabunge kwa kuwataka viongozi hao kuwahudumia wananchi waliowachagua kwanza kabla ya kudai nyongeza ya mishahara.

    0 Responses

    Posted on May 14, 2013 na Mate Tongola

  • JAB

    Watakaojiunga na Vyuo Kuongezeka

    Bodi ya uteuzi wa wanafunzi wanaojiunga na vyuo vikuu vya umma, imeweka kiwango kipya cha alama ya wastani, ya wanafunzi kujiunga na vyuo vikuu vya umma nchini. Kwa mujibu wa bodi hiyo, wavulana waliopata B kuanzia alama 61 kwenye mtihani wa KCSE uliofanywa mwaka jana watateuliwa, huku wasichana waliopata B hasi yenye alama 59 wakiteuliwa. Hatua hii inamaanisha kuwa idadi ya wanafunzi watakaojiunga na vyuo hivyo itakuwa 53,010 kutoka idadi ya wanafunzi 42,000 mwaka uliotangulia, hili likiwa ongezeko la wanafunzi 11,000. Bodi hiyo aidha imetangaza kuwa jumla ya wasichana 2,794 watateuliwa kujiunga na vyuo vikuu katika juhudi za kuongeza idadi ya wanafunzi wa jinsia ya kike wanaojiunga na taasisi za juu za elimu, huku wengine 94 kutoka maeneo kame wakitengewa nafasi hiyo.

    0 Responses

    Posted on May 13, 2013 na Geoffrey Mung'ou

  • Usalama

    Watakiwa kusalimisha silaha - Mandera

    Wakazi wa kaunti ya Mandera wana hadi kesho kusalimisha silaha haramu la sivyo wapokonywe kwa nguvu na serikali. Maafisa wakuu wa usalama wakiongozwa na Inspekta mkuu wa Polisi David Kimaiyo, Naibu wake Grace Kaindi, Mkurugenzi wa Idara ya Upelelezi wa Jinai Ndegwa Muhoro ambao wamezuru Kaunti ya Mandera wamesema kuwa watakaokiuka agizo hilo watakabiliwa kisheria. Tayari mafisa 200 zaidi wa polisi wametumwa eneo hilo kushika doria. Ni jumamosi wiki iliyopita ambapo mashambulizi mengine yalizuka katika eneo hilo, ambapo afisa mmoja wa polisi aliuawa. Mauji hayo yanasemekana yalisababishwa na kundi la washambuliaji ambao walitupa vilipunzi ndani ya kituo cha polisi. Maafisa wanne ambao walijeruhiwa katika shambulizi hilo, wangali wanapokea matibabu katika hopsitali moja mjini Mandera. Wakazi wamedai kwamba mapigano hayo ni kati ya jamii mbili za Degodia na Gareh. Kufikia sasa watu 4 wameuawa huku wengine elfu 4 wakitoroka makwao.

    0 Responses

    Posted on May 13, 2013 na Mate Tongola

  • Usalama

    Walio na akili tahira watoroka Hospitalini

    Polisi jijini Nairobi wanawasaka wagonjwa 40 wa akili waliotoroka kutoka hospitali ya Mathari mapema jumatatu. OCPD wa Starehe Samuel Anampiu ameiambia Radio Maisha kwamba 40 hao walikuwa miongoni mwa 75 waliotoroka kutoka chumba walimokuwa wamefungiwa. Hata hivyo, 35 kati yao walikamatwa baada ya jaribio lao la kutoroka kutofua dafu. Aidha, tisa kati ya waliotoroka wamerudishwa hospitalini humo na jamaa zao, huku 7 wakijirejesha wenyewe. Anampiu ameongezea kwamba 40 hao walifanikiwa kutoweka baada ya kuwazidi nguvu walinzi waliokuwa wakilinda hospitali hiyo ya wagonjwa wa akili. Inaaminika kuwa wagonjwa hao walikuwa wakilalamikia dawa ambazo walikuwa wamepewa wakisema kuwa haziwasaidii. Msako dhidi yao umeimarishwa hadi katikati mwa jiji na viunga vyake.

    0 Responses

    Posted on May 13, 2013 na Mate Tongola

  • Waliochujwa

    Ripoti ya Uchujaji

    Kamati ya bunge inayohusika na uteuzi wa mawaziri na makatibu inaendelea na shughuli ya kuandaa ripoti itakayowasilisha bungeni kuhusu shughuli ya kuwachuja mawaziri wateule. Wanakamati hao 28 wanakutana katika hoteli ya Windsor hapa Nairobi ambako wanalinganisha nyaraka walizopata kutoka kwa wananchi na utetezi uliotolewa na watahiniwa. Kutokana na hayo kamati hiyo itafikia uamuzi wa kupendekezwa wateuliwe au kupinga uteuzi wao. Kiongozi wa walio wengi bungeni Aden Duale amepangiwa kuwasilisha ripoti hiyo katika kikao cha jumanne alasiri ambapo bunge linatarajiwa kuwajadili na kuwaidinisha au kuwakataa wateule hao. Muda wa siku 14 ambazo bunge linafaa kutumia kuwatathmnini wanaopendekezwa na rais unakamilika usiku wa manane kesho na hivyo bunge linafaa kufanya uamuzi wake kufikia wakati. Iwapo halitaweza basi rais atakuwa huru kuwateua rasmi mawaziri hao bila kuzingatia mtazamo wa bunge.

    0 Responses

    Posted on May 13, 2013 na Benard Oginga

  • Mishahara

    Tume ya Mishahara kutotikisika

    Tume ya Mishahara SRC imesema haitalegeza msimamo wake kuhusu hatua yake ya kupendekeza mishahara mipya kwa wabunge. Katika mkutano na wanahabari, mwenyekiti wa tume hiyo Sarah Serem amesisitiza kwamba uchumi wa Kenya bado kunawiri ifaavyo kwa hivyo haiwezi kugharamia mishahara ya kiwango wanachotaka wabunge. Serem amedokeza kuwa kabla ya kuifanyia mabadiliko mishahara hiyo, SRC ilifanya uchunguzi kote ulimwenguni pamoja na kutathmini uchumi ya mataifa mbali mbali ikiwemo iliyostawi. Aidha, Serem amesema tume yake haitotishwa na wabunge wanaodai kuwa na uwezo kuibandua tume hiyo. Kwa mujibu wa SRC, taifa la ufaransa hupata pato ambalo ni zaidi ya la Kenya kwa mara ishirini na hali mshahara wa mbunge nchini humo ni sawa na shilingi nusu milioni za Kenya. Vile vile, katika mataifa jirani wabunge nchini Rwanda hulipwa mshahara ambao ni sawa na shilingi alfu 173, huku Tanzania wakipata mshahara uliosawa na shilingi alfu 79.

    0 Responses

    Posted on May 13, 2013 na Mate Tongola