Usalama
Visa vya Uhalifu kukomshwa - Uhuru
Rais Uhuru Kenyatta amewataka makamanda wa polisi kuwachukulia hatua za sheria wale wote watakaohusishwa na vitendo vya utovu wa usalama nchini. Katika mkutano ulioandaliwa katika ikulu ya Rais hapa Nairobi, Uhuru amesisitiza kwamba serikali yake yaitoruhusu utepetevu katika idara ya polisi. Ametoa agizo hilo wkaati kumekuwa na tetesi kwamba baadhi ya wanasiasa wanahusika pakubwa kwenye mashambulizi na mauaji yaliyoshuhudiwa katika kaunti za Busia na Bungoma wiki iliyopita. Duru kutoka mkutano huo wa alhamisi zimearifu kwamba wakuu hao wa polisi walimwarifu rais kuwa wanakabiliwa na changamoto kadhaa ikiwemo ukosefu wa vifaa vya kazi, kutokuwepo kwa motishia miongoni mwa polisi na kadhalika. Vile vile, mafisa hao wamemtaka rais Uhuru kusitisha mabadiliko yanayofanyiwa idara hiyo ikiwemo kuteuliwa kwa makamanda wa kaunti. Hata hivyo, Uhuru amewahakikishia wakuu hao kwamba atashirikiana nao kikamilifu ikiwemo kushughulikia kwa haraka chamgamoto zinazowakabili.
Posted on May 17, 2013 na Mate Tongola
