Tangu kutumwa kwa maafisa wa polisi katika eneo la tana delta kwa lengo la kuimarisha usalama pamoja na kuwapokonya wenyeji silaha haramu zilizo mikononi mwao wenyeji hao wamelalamika kwa kusema kuwa maafisa wa polisi wamekuwa wakiwanyanyasa kwa kuwaadhibu pamoja na kutumia nguvu kupita kiasi. Mbunge wa eneo hilo Danson Mungatana amelitaka zoezi hilo la kutafuta silaha haramu kusitishwa huku akiwataka walinda usalama kutekeleza majukumu yao kwa mujibu wa sheria